Language

Mradi wa OMDM unalenga kuimarisha uwezo wa ufuatiliaji wa mwenendo wa maambukizi ya ugonjwa wa malaria katika ngazi zote za Serikali ya Tanzania (GoT), kuongeza ubora wa matokeo ya afua zinanzotumika dhidi ya Malaria kwa kuboresha ulengaji  na utekelezaji wa afua kwenye maeneo husika, kuboresha mbinu za kudhibiti vyanzo vya maambukizi na kukabiliana na milipuko, na kutoa takwimu muhimu kwa serikali na wadau kwa ajili ya maendeleo na maamuzi ya  kisera ya mpango wa kudhibiti malaria.