Language

Licha ya maendeleo na juhudi za serikali katika kutatua tatizo la lishe duni, utapiamlo bado ni tatizo nchini Tanzania. Kupitia mradi wa Lishe Endelevu, Serikali ya Marekani itachangia lengo hili la taifa kwa:

  • Kupunguza udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka 5 katika mikoa minne.
  • Kuongeza idadi ya wanawake walio katika umri wa kuzaa kula vyakula vyenye mchanganyiko kwa kiwango kinachokubalika.
  • Kuongeza idadi ya watoto wenye umri wa miezi 6-23 kula vyakula vyenye mchanganyiko sahihi na kwa nyakati sahihi.